Msemaji wa Shirika la umeme Tanzania (TANESCO), Eng. Kenneth Boymanda amesema umeme utaanza kurejeshwa kwa awamu katika maeneo uliyokatika kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye gridi ya Taifa.
Amesema baadhi ya mikoa tayari huduma hiyo inarejea na kuongeza kuwa Mikoa ya Singida, Dodoma na Tanga itaanza kabla ya Dar es salaam.


