Papa Leo alitembelea msikiti wa The Blue Mosque huko Istanbul siku ya Jumamosi, na kuvua viatu vyake kama ishara ya heshima lakini hakushiriki sala wakati wa ziara hiyo. Hii ni ziara yake ya kwanza kama kiongozi wa kanisa Katoliki katika eneo la ibada ya dini ya kiislamu.

Msikiti huo wenye uwezo wa kuchukua waumini 10,000, ulionyeshwa kwake na imamu na mufti wa Istanbul. Akiwa amevaa soksi nyeupe, Leo alitabasamu, kutaniana na muezzin mkuu wa msikiti huo, na kuonyeshwa muonekano wa msikiti huo kwa takribani dakika 20.


