Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Samia Suluhu Hassan imempendekeza Deogratius Ndejembi (43) kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Asha-Rose Migiro, alitangaza uamuzi huo usiku wa Jumatano, Agosti 26, 2026, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.
Dkt. Migiro amesema jina la Ndejembi litapelekwa Bungeni kwa hatua zinazofuata.

