Bei ya mafuta ya petroli imepanda kwa Jiji la Dar es Salaam toka shilingi 3,820 kwa lita mwezi Aprili hadi kufikia shilingi 4115 kwa lita mwezi Mei 2026, kulingana na taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).
Upandaji huo unaonesha kuwa imeongezeka kwa shilingi 295 ikiwa ni mwendelezo wa mafuta kupanda.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa kupanda kwa bei kunatokana na mabadiliko ya soko la Kimataifa, likiwemo ongezeko la bei ya mafuta ghafi na changamoto za usafirishaji.
Aidha, hali ya kisiasa na kiusalama duniani, hususan mvutano unaoendelea kati ya mataifa mbalimbali, imechangia

