Shirikisho la soka nchini Guinea limewaomba CAF kufanya marejeo ya mchezo wa fainali ya Afcon mwaka 1976 kati yao na Morocco
Mwaka huo ilichezwa fainali ya Afcon ambapo dakika ya 33 wachezaji wa Morocco waliondoka kwenye mechi kwa dakika 15 na kurudi tena huku sababu kuu iliyofanya waondoke ni baada ya mwamuzi Nyirenda Chayu kumpa kadi nyekundu Abdallah Semmat baada ya kumfanyia madhambi hatari Papa Camara
Shirikisho la mpira la Guinea linasema kama Morocco watapewa ubingwa wa 2025, sio kosa na wao wakipewa ubingwa wa 1976 kwani Morocco walitoka nje ya uwanja na kurudi uwanjani na kushinda mchezo huo.
Mdau wewe una maoni gani kuhusiana na hili sakata?


